Politics
Namna Raila Ameichanganya Jamii Ya Mlembe

Eneo la magharibi limegawanywa na kugeuzwa ngome ya wageni. Tangu kifo cja aliyekuwa makamu wa Rais wa Kenya Michael Kijana Wamalwa, Jamii ya Mulembe imeshindwa kupanda mchongoma ili kupata kiti cha juu cha Urais. Miaka nenda miaka rudi, jamii hiyo imekuwa ikimuunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga kama alivyodokeza kinara wa ANC Musalia Mudavadi.
Wito wa baadhi ya wakazi na viongozi wa eneo hilo kubuni chama kimoja umesambaratika na umezikwa kwenye kaburi la sahau. Mapinduzi kwenye chama cha Ford Kenya tena yanakadiriwa kwenye ANC yameigawanya jamii ya Luhya. Mmoja wa kinara wa NASA, Wetangula amepoteza wadhifa wake na hivyo kushusha matumaini yake kabisa na chama.

PICHA; Musalia Mudavadi
Weta amemlaumu Raila kwa yanayoshuhudiwa eneo la magharibi na amemtaka kinara huyo kuiwacha jamii ya Mulembe. Mkutano ulioandaliwa nyumbani pa katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli, ulizua tumbo joto na sasa mipango yake inaonekana.
Mkutano huo ulihudhiriwa na wabunge, maseneta, magavana na hata waziri Eugene. Gavana wa Kakamega alitwikwa jukumu pamoja na Atwoli ya kuiongoza jamii hiyo kisiasa ili kurudisha hadhi ya eneo hilo. Baada ya mkutano huo, chama cha ODM kilifanya mageuzi kwenye mabaraza mbalimbali ya bunge na wengi wa wabunge kutoka eneo la magharibi waliathirika kwa kuwa washirika wa karibu wa Naibu wa Rais.
Naibu kiranja wa wachache Chris Wamalwa alipoteza kiti chake kilichonyakuliwa na Eseli Simiyu mbunge wa Tongaren. Hali hii ikasababisha tena msukomsuko ndani yachama cha Ford Kenya ambapo Chris aliteuliwa kuwa katibu mkuu wa chama na Eseli kutemwa. Huu ndio ulikuwa mwanzo na mwisho wa Weta kwani Eseli pamoja na Wafula Wamunyinyi walifanikisha kumbandua kama kinara wa chama hicho.
Toa Maoni, Shirikisha, Na Fuata Kwenye tovuti stateupdate.co.ke Kupata Habari Zaidi
-
News4 weeks ago
What Killed Tanzanian President John Magufuli
-
News4 weeks ago
Panic As Covid-19 Takes Two Family Members At The Same Time
-
News4 weeks ago
R.I.P Popular Royal Media Journalist Dies
-
World News1 week ago
Fearless Suluhu Reveals The Covid-19 Truth To Tanzanians, Overturns Magufuli’s Rules
-
Crime4 weeks ago
Tension: Heavily Armed Alshaabab Terrorists Take Over A Town
-
Health & Fitness3 weeks ago
Family Member Reveals Details On Raila’s Health
-
Politics3 weeks ago
R.I.P Ruto Thrown Into Deep Mourning
-
News3 weeks ago
Big Blow To Baba? How Uhuru Is Playing Raila In Favour Of Ruto